Diamond Platnumz ameamua kufunguka ya moyoni kuhusiana na kile alichokieleza kama kusemwa vibaya na wasanii wenzake ilihali yeye amekuwa akifanya mambo kimpango wake.
“Kiukweli, nasikitishwa sana jins baadhi ya wasanii kutwa wanavyolazimisha kunitengenezea ugomvi wa kilazima pasipo kuwa na sababu, mara wengine wakizusha eti Nimewatusi kwenye Media, Mara sjui Nimepost kuwakashif, yaani ilimradi tu….kwanini Wanamuziki wa Tanzania Tunashindwa kubadilika… mbona mi nahangaika na muziki wangu kimpango wangu…” Mnasema nyie ndio mnaojua kuimba mie sijui “sinatatizo… Mnasema nyie ndio wenye sauti nzuri yangu mbaya “Sina tatizo”… sasa mbona tena bado mnanifatilia na kutokujua kwangu… Nafkiri ni vyema mkaanza kutumia ujuzi wenu kukuza sanaa ya nchi yetu na kuleta heshima na maendeleo nchini, kuliko kupika majungu….. Watu wanataka kazi,” ameandika kwenye Instagram.
No comments:
Post a Comment