expr:class='"loading" + data:blog.mobileClass'>

Tuesday, June 18, 2013

"CCM WALITAKA KUNIUA KWA MLIPUKO WA BOMU JIJINI ARUSHA".....MBOWE

MWENYEKITI Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),Freeman Mbowe amesema tukio la mlipuko wa bomu lililoua watu wawili juzi mkoani Arusha, lilimlenga yeye na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Arusha jana, Mbowe alisema bomu hilo ambalo liliambatana na milio ya risasi lilikusudiwa wazi kuondoa uhai wake, jambo ambalo ni hatari kwa uhai wa taifa.


Alisema katika tukio hilo, kulikuwa silaha za aina tatu ambazo zilitumika, ukiondoa bomu, kulikuwa na bunduki aina ya Sub Machine Gun (SMG) na bastola.

“Waliopanga unyama ule walilenga kutuua sisi, waliokufa wamekufa kwa niaba yetu,

“Watu hawa, waliandaliwa na wengine walikuwa katikati ya umati wa watu, waliokuwa pembezoni mwa uwanja, tumebaini wanalindwa na polisi,


“Risasi za SMG zilitoboa tanki la mafuta la gari letu la matangazo, ambalo sisi tulikuwemo juu, lengo likiwa baada ya bomu kulipuliwa,tanki nalo lingelipuka,

“Hawa walitaka kufanya mauaji halaiki, ikiwemo sisi viongozi wa Chadema, Mungu bado anatusimamia,”alisema

Alisema majeruhi wote ambao wamelazwa, bado wana vyuma vingi milini mwao kutokana na kujeruhiwa vibaya.

“Tumepiga picha makasha ya risasi na kuyakabidhi polisi,bado tunaamini,kwa sababu tukio hili halihitaji mashine ya kiuchunguzi ya mwezini vyombo vya usalama, vitatoa taarifa mapema,”
alisema Mbowe.

Kutokana na msiba huo, Mbowe alitangaza kuwa wabunge wa chama hicho, wote kuanzia leo hawatashiriki mkutano wa Bunge la Bajeti hadi marehemu watakapozikwa.

“Msiba huu, umekigusa chama,wanachama,wapenzi na wananchi wote wa Tanzania,wabunge wote watakuwa bega kwa bega na wananchi wa Arusha mpaka watakapopumzishwa marehemu,”alisema Mbowe

Alisema mazishi ya marehemu wote, yatafanyika kitaifa kwenye Viwanja vya Soweto, kabla ya marehemu wote kusafirishwa na ndugu zao.

“Chama kinauchukulia msiba huu kama msiba wa taifa,tumeamua kupiga mahema katika uwanja ule na marehemu wataagiwa hapo ambapo moja ni atazikwa Kilimanjaro na mwingine Tabora”

“Tukio hili ni la kisiasa na limepangwa, ninawataka wenzetu kama shughuli za siasa zimewashinda wafute mfumo wa vyama vingi ili wananchi wasio na hatia wasiendelee kufa”


Alisema chama kitafanya harambee kuchangia majeruhi kwa ajili ya matibabu yao.

No comments:

Post a Comment