expr:class='"loading" + data:blog.mobileClass'>

Sunday, April 27, 2014

Mfahamu vizuri mwigizaji Jacob Steven (JB). Ametoka wapi na historia yake yote kwa ufupi mpaka sasa



Baada ya miaka 13 ya kuwapo katika fani ya sanaa ya maigizo, hakuna shaka kwamba, Steven Jacob maarufu kama JB, kwa sasa ni miongoni mwa watu wenye majina makubwa mno katika fani hiyo nchini. Ni miongoni mwa nyota `Watano’ Bora zaidi wa kiume kwa upande wa fani hiyo, hivyo kumfanya kuwa katika hadhi ya juu, sawa na nyota wengine kama akina Steven Kanumba na Vincent Kigosi `Ray’ na wengine.
Ndiyo maana haishangazi kuona kwamba, hata leo hii ukiingia katika soko la filamu zilizo juu, huwezi kukosa kazi za nyota huyo. 
Kwa sasa, JB, mtu mwenye umbo la miraba minne licha ya kucheza filamu ni mwandishi wa filamu na mtayarishaji, anatamba na ‘Illegal Sisters’, ‘Signature’, ‘Tanzanite’ na ‘Msamaha wa Rais’, Nakwenda kwa mwanagu, Dereva tax D.N.A na nyingine nyingi. 

Katika mahojiano na tovuti hii hivi karibuni, JB anasema kwamba, ana kila sababu ya kujivunia mafanikio yake, ingawa hawezi kuvimba kichwa kwa umaarufu, huku akisisitiza alianza kuigiza kama mzaha na baadaye taratibu fani ikamkolea na kuigeuza sehemu ya maisha yake. 
Anasema kwamba, alikuwa `anaburuzwa’ na